Friday, February 15, 2013

UWEKEZAJI WA NCHI YA CHINA AFRIKA



UWEKEZAJI WA NCHI YA CHINA AFRIKA

 Nchi ya china imewekeza katika sekta mbalimbali Afrika, ambapo imewekeza katika sehemu zifuatazo:

1/MIUNDOMBINU 
Hapa imewekeza katika ujenzi wa barabara,viwanja vya ndege,bandari,hospitali pamoja na shule

2/BIASHARA
Nchi ya ya china imekuwa ikifanya biashara ya kuuza,simu za mkononi,luninga,radio,nguo pamoja na viatu ambapo vitu hivi vimekuwa vikkuuzwa kwa bei rahisi kuliko biashara kutoka makampuni mengine ya ndani na nje ya nchi.

3/KILIMO
Halikadhalika pia wamewekeza katika kilimo ili kupata malighafi ya kutengenezea bidhaa zao kama vile pamba
.
4/MADINI
Hii ndio sekta ambayo wamewekeza zaidi  kwasababu wanatumia madini zaidi katika utengenezaji wa bidhaa zao kama vile simu za mkononi ambapo wanachukua madini mengi zaidi kutoka nchi ya Zimbabwe, Zambia na  Afrika kusini.

AFRIKA WANAFAIDIKA NINI?
FAIDA
Kwaupande mwingine kuna faida lakini pia kuna hasara,
Nikianza na faida katika upande wa miundombinu kama  barabara nk, Afrika inafaidika kwasababu barabara  au bandari ambazo wanajenga wachina ziko katika ubora unaotakiwa.
Nchi ya china imekuwa ikijenga shule,kuchimba visima pamoja nakutoa madawati,lakini pia wa Afrika wengi wamekuwa wakipata nafasi ya kusoma katika nchi ya china.
Pia china imekuwa ikileta madaktari Afrika aidha kwaajili ya kufanya mafunzo au kuajiriwa katika nchi za Afrika.
Waafrika wamekuwa wkifaidika na bidhaa zao kwasababu zinauzwa kwa bei rahisi kuliko bidhaa ambazo zinauzwa ndani ya nchi kama vile nguo na simu.

HASARA
Afrika wamekuwa wakipata hasara hasa katika viwanda kwasababu waafrika wanapenda vitu vya bei rahisi kwahiyo wanakimbilia kununua bidhaa za kichina kwasababu  vinauzwa kwa bei rahisi na kuacha vya kiafrika kwasababu ni ghali.
Lakini pia waafrika wamekuwa wakipata hasara kwasababu wanapenda vitu vya bei rahisi lakini havidumu kama vile simu.








No comments:

Post a Comment